Saturday, October 31, 2015

Kitunguu Swaumu hutibu magonjwa 30

MUNGU anaposema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa hamaanishi maarifa ya kutengeneza au kuendesha ndege, ni maarifa ya kawaida tu katika maisha yetu ya kila siku ambayo yanaweza kubadilisha afya na ustawi wetu. Moja ya mmea ambao umependelewa sana na Mungu kwakuwa na viinilishe vingi na mhimu sana kwa afya ya binadamu ni kitunguu swaumu. Kitunguu swaumu ni dawa karibu kwa kila ugonjwa.
Huko sokoni tayari nimeviona vitunguu swaumu kutoka China na Afrika kusini ambavyo vyenyewe huwa vina punje kubwa nene na huwa rahisi kuvimenya, hata hivyo ili upate faida hizi zote hapa chini naendelea kukushauri utumie vitunguu swaumu vyetu vinavyolimwa hapa Tanzania kwani hivyo vya kutoka nje pamoja na kuwa ni rahisi kuvimenya lakini ubora wake si kama ule wa vitunguu vyetu.
Hakikisha kila mboga unayopika haikosi kitunguu swaumu ndani yake na ikibidi ukiweke mwishoni mwishoni unapokaribia kuipuwa mboga yako toka katika moto kwamba kisiive sana hata kupoteza viinilishe vyake. Kama una friza au friji ya kawaida unaweza kumenya vitunguu swaumu hata kilo nzima na kuvitwanga kidogo katika kinu, vifunge vizuri katika bakuli au mfuko wa plastiki na uvihifadhi katika friza au friji na hivyo kila unapopika unachukuwa tu na kukitumia ili kuepuka usumbufu wa kukimenya kila siku.
Lakini ili upate faida zaidi za kitunguu swaumu utatakiwa ukimeze katika majikikiwa kibichi, yaani bila kupitishwa katika moto au kuwa kimepikwa.
Chukuwa kitunguu swaumu kimoja
kitunguu swaumu
kitunguu swaumu

Kigawanyishe katika punje punje
kitunguu swaumu
kitunguu swaumu

Menya nusu yake (punje 8 au 10 hivi),
kitunguu swaumu
kitunguu swaumu

Menya punje moja baada ya nyingine
kitunguu swaumu
kitunguu swaumu

Kisha vikatekate (chop) vipande vidogo vidogo na kisu
kitunguu swaumu
kitunguu swaumu
Meza kama unavyomeza dawa na maji vikombe 2 kila unapoenda kulala au fanya kutwa mara 2 kama unaumwa na moja wapo ya magonjwa niliyoyaorodhesha hapa chini.
Fanya hivi kila siku au kila mara unapopata nafasi na hivyo utakuwa mbali na kuuguwauguwa. Mama mjamzito chini ya miezi 4 ni vema asitumie, kwa ujumla tu mjamzito uwe makini utakapotumia kitunguu swaumu kwa namna hii kama wewe ni mjamzito.
kitunguu swaumu
Kitunguu swaumu kilichokatwakatwa/chopped

Kitunguu swaumu hutibu magonjwa 30

Haya ni baadhi ya magonjwa yanayotibika au kukingika na kitunguu swaumu:
  1. Huondoa sumu mwilini
  2. Husafisha tumbo
  3. Huyeyusha mafuta mwilini (kolestro)
  4. Husafisha njia ya mkojo
  5. Hutibu amoeba, minyoo na Bakteria
  6. Huzuia kuhara damu (Dysentery)
  7. Huondoa Gesi tumboni
  8. Hutibu msokoto wa tumbo
  9. Hutibu Typhoid
  10. Huondoa mabaka mabaka kwenye ngozi
  11. Hutibu mafua na malaria
  12. Hutibu kifua kikuu
  13. Hutibu kipindupindu
  14. Hutibu upele
  15. Huvunjavunja mawe katika figo
  16. Hutibu mba kichwani
  17. Huupa nguvu ubongo
  18. Huzuia meno kung’ooka na kutuliza maumivu
  19. Huongeza SANA nguvu za kiume
  20. Hutibu maumivu ya kichwa
  21. Hutibu kizunguzungu
  22. Hutibu shinikizo la juu la damu
  23. Huzuia saratani/kansa
  24. Hutibu maumivu ya jongo/gout
  25. Huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula
  26. Huongeza hamu ya kula
  27. Huzuia damu kuganda
  28. Husaidia kutibu kisukari
  29. Husaidia kutibu tatizo la kukosa usingizi
  30. Huongeza SANA kinga ya mwili
Share:

0 comments:

Post a Comment

Top Servicare. Powered by Blogger.

Web Design

Popular Posts

INSTAGRAM FEED

@soratemplates

Blog Archive

About