Wednesday, November 4, 2015

ZIJUE FAIDA NNE ZA KUJENGA NYUMBA KWA KUTUMIA RAMANI YA NYUMBA


Ramani ni neno lililozoeleka masikioni mwa watu wengi kwa waliosomea fani hiyo ya ramani na hata kwa watu ambao hawajasomea fani hiyo kutokana na ukweli kwamba ramani hutumika kila siku katika maisha yetu ya kila siku na hakuna uwezekano wa kulipinga hili.

Mfano: Wewe ni mwenyeji katika eneo fulani na unamfahamu mzee mmoja katika eneo hilo anaitwa Mzee Mwamba, basi mara ukakutana na mtu mmoja akakauulizia kuhusu mzee huyo na akakuomba umwelekeze mahali anapoishi mzee huyo, bila shaka utaanza kumwelekeza: nyooka na barabara hii kama mita hamsini hivi mbele utaona barabara inakunja kona kuelekea kulia nenda nayo hiyo barabara kama mita miambili hivi utaona jengo kubwa jeupe mkono wa kushoto halafu mkabala na jengo hilo utaona  duka la vifaa vya ujenzi, uliza hapo dukani watakuonesha nyumba ya huyo mzee.


Hayo maelekezo uliyoyatoa ni ramani sema tu hujaichora na ukiamua kuichora utaiona kama zilivyo ramani za kawaida.
Kwa mantiki hiyo kila mtu kichwani mwake ana ramani nyingi sana nzuri zenye manufaa kwake na kwa taifa kwa ujumla na laiti ramani hizo zingechorwa  tungekuwa na maktaba kubwa ajabu na wakati mwingne hata sehemu ya kuhifadhi zisingetosha.

Maisha ya kila siku.
Unapotaka kuishi kwako yaani katika nyumba yako mwenyewe kuna ramani ya nyumba yako ungependa iwe yaani mwonekano, rangi, ukubwa na hata mwelekeo (orientation) wake. Ungependa umpate mtu mwenye uwezo wa kuionesha ramani hiyo iliyoko kichwani mwako na kisha uipate na uanze hatua  ya kuijenga ili uipate ile furaha unayodhani utaipata mara nyumba hiyo itakapo kamilika.



Itakusaidia kukadria gharama za ujenzi.
Maadamu  ramani hiyo itakuwa imeonesha vipimo vya “material” ya ujenzi itakuwa rahisi kujua idadi ya bati, matofali, madirisha,nk hii itasaidia kukufanya ujipange vizuri kabla ya kuanza ujenzi.

Ni kiambatisho muhimu katika kupata kibali cha ujenzi.
Kwa mujibu wa sheria ya ujenzi wa majengo  inataka ili mtu apate kibali cha ujenzi wa jengo lolote ni lazima aambatanishe katika maombi yake ramani ya jengo analotaka kujenga. Ramani hii itasainiwa na Afisa mipango miji, afisa ardhi na bwana afya na kamati ya ujenzi ya wilaya/mji/manispaa/jiji. nk

Ramani ya nyumba ni kielelezo muhimu katika taasisi za mikopo.
Ukitaka kuchukua mkopo benki au katika taasisi za mikopo na hasa ukitaka kuweka nyumba kama dhamana watahitaji kuiona ramani ya nyumba yako na watahitaji kuiambatanisha katika barua yako ya maombi ya mkopo huo.

Hizo ndizo faida kuu nne za kujenga nyumba kwa kutumia ramani ya nyumba ingawaje zinaweza kuwepo nyingine nyingi, ikumbukwe kuwa kujenga nyumba bila ramani ni sawa na kulima shamba kubwa bila kujua utapanda nini katika shamba hilo, ni hatarii.






TOPSERVICECARE tunaamini kuwa “Kile akili ya binadamu inakiwaza na kukiamini, akili ya binadamu inaweza kukipata”.Na tena, Mtu mmoja mwenye ujasiri ni watu wengi


Tunakuhamasisha ili ufikie mafanikio yako
Share:

0 comments:

Post a Comment

Top Servicare. Powered by Blogger.

Web Design

Popular Posts

INSTAGRAM FEED

@soratemplates

Blog Archive

About